Jamaa Wa miaka hamsini Na Tisa (59) kutoka Migori amefariki baada ya kumeza Viagra ili kujiandaa kabisa kabla ya kupatana Na mwanamke waliyepanga naye kupatana, ambaye baadae kageuza mipango yote.
Kulingana na habari kutoka Kwa Polisi, jamaa huyu hakujua kwamba mwanamke yule alikuwa kwenye siku zake za hedhi, na basi akaandaa mahali ambapo wangejiburudishia baada ya kupatana.
Inasemekana kwamba baada ya kutafuta chumba katika Bar ya Urembo Kata ndogo ya Ntimaru, mpango wake Wa kando aliwasili, marehemu alimwagizia soda Na mkate kwenye mgahawa akawa anamsubiri wakaanze mambo yao.
Mambo yaligeuka wakati mpango Wa kando alisema kwamba yupo kwenye siku zake za hedhi na kabisa hawezi shiriki mapenzi naye.
Baada ya muda mchache jamaa akazidiwa Na kufariki.